Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA–, Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema kuwa Hati ya Maelewano (Memorandum of Understanding) kati ya Iran na Marekani kwa sasa inapitia hatua ya mgogoro kutokana na kile ilichodai kuwa ni ukiukaji wa mara kwa mara unaofanywa na Washington.
Katika taarifa yake, wizara hiyo imesisitiza kuwa Iran haitakuwa upande wa kwanza kukiuka makubaliano hayo, ikieleza kuwa Marekani imekuwa ikivunja ahadi zake mara kwa mara.
Aidha, Tehran imesema haitaruhusu Marekani na Israel kutumia Mlango-Bahari wa Hormuz kwa namna yoyote itakayodhuru Iran au kuhatarisha mamlaka na uhuru wake wa kitaifa.
Wizara hiyo pia imeishutumu Washington kwa kukiuka mara kwa mara Kifungu cha Tano (Article V) cha Hati ya Maelewano, ikidai kuwa hatua hizo zimehatarisha usalama wa usafiri wa baharini na kuchangia kuongezeka kwa mvutano katika eneo.
Iran imesisitiza kuwa kuheshimu makubaliano na kutekeleza ahadi ni msingi muhimu wa uhusiano wa kidiplomasia, na kwamba ukiukaji wa masharti ya makubaliano unaweza kuathiri juhudi za kupunguza mvutano na kuimarisha utulivu wa kikanda.
Maoni yako